sw_tn/rev/19/09.md

854 B

Taarifa ya Jumla:

Malaika anaanza kuzungumza na Yohana. Hii inawezekana kuwa malaika yule yule aliyeanza kuzungumza na Yohana katika 17:1.

walioalikwa

Unaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "watu ambao Mungu amewakaribisha"

sherehe ya harusi ya Mwana kondoo

Hapa malaika anazungumzia kuunganishwa kwa Yesu na watu wake kama vile ni sherehe ya harusi.

Nilisujudu

Kusujudu ni kula chini kwenye ardhi, uso ukitazama chini, kuonesha heshima na utayari wa kutumika.

ndugu zako

Neno "ndugu" hapa inamaanisha waumini wote wa kiume na wa kike.

wenye kuushika ushuhuda wa Yesu

Hapakushika inamaansiha kuamini au kutangaza. "wanaosema ukweli kuhusu Yesu"

kwa kuwa ushuhuda wa Yesu ni roho ya unabii

Hapa "roho ya unabii" inamaanisha Roho Mtakatifu wa Mungu. "kwa sababu ni Roho wa Mungu anayewapa watu nguvu ya kunena ukweli kuhusu Yesu"