sw_tn/rev/18/23.md

1.1 KiB

Kauli Unganishi:

Malaika aliyetupa jiwe la kusagia anamaliza kuongea.

Taarifa ya Jumla:

Maneno "yako," "wako," na yake" inamaanisha ni Babeli.

Sauti ya bwana harusi na bibi harusi hazitasikiwa tena ndani yako

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Hakuna ambaye atasikia tena ndani ya Babeli sauti za furaha za bwana harusi na bibi harusi"

hazitasikiwa tena ndani yako

"hakuna atakaye visikia ndani yenu tena." Kutosikiwa hapa inamaanisha havitakuwepo" "havitakuwa ndani ya mji wenu tena"

wafanyabiashara wako walikuwa wakuu wa nchi

Malaika anazungumzia watu muhimu na wenye nguvu kama vile walikuwa wana wa wafalme. "wafanya biashara wenu walikuwa kama wana wa waflame duniani" au "wafanya biashara wenu walikuwa watu muhimu zaidi duniani"

mataifa, wamedanganywa kwa uchawi wako

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "uliwadanganya watu wa mataifa na uchawi wako"

Ndani yake damu ya manabii na waamini ilionekana, na damu ya wote waliouawa juu ya nchi

Damu kukutwa ndani yake ina maana kuwa watu walikuwa na hatia ya kuua watu. "Babeli inahatia ya kuua manabii na waumini na watu wengine wote waliouawa"