sw_tn/rev/18/21.md

1.3 KiB

Kauli Unganishi:

Malaika mwingine aanza kuzungumzia Babeli. Huyu ni malaika tofauti na yule aliyezungumza awali.

jiwe kuu la kusagia

Jiwe kubwa la duara linatumika kusaga nafaka.

abeli, ule mji mkuu, utatupwa chini kwa nguvu na hautaonekana tena

Mungu atauangamiza ule mji kikamilifu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu ataitupa Babeli kwa nguvu, ule mji mkuu, na haitakuwepo tena"

hautaonekana tena

"na hakuna mtu atakayeuona tena." Kutokuonekana hapa inamaanisha kwamba haitakuwepo tena. "haitakuwepo tena"

Sauti ya wapiga vinanda, wanamuziki, wacheza filimbi, na tarumbeta hawatasikika tena kwenu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Hakuna mtu katika mji wenu ambaye atasikia tena sauti ya wapiga vinanda, wanamziki, na wacheza filimbi, na sauti ya tarumbeta"

kwenu

Malaika anazungumza kana kwamba Babeli alikuwa hapo akimsikiliza. "ndani ya Babeli"

hawatasikika tena kwenu

"hakuna mtu atakayewasikia tena." Kutosikiwa hapa inamaana ya kutokuepo. "hawatakuwepo katika mji wenu tena"

Hakuna fundi ... hataonekana kwenu

Kutopatikana humo inamaana hawatakuwemo. "Hakuna fundi yeyote atakaye kuwa katika mji wenu"

Hakuna sauti ya kinu itakayosikika tena kwenu

Sauti ya kitu kutokusikika inamaana kwamba hakuna atakaye sikia hiyo sauti. "Hakuna atakaye tumia vinu katika mji wenu"