sw_tn/rev/18/15.md

1.3 KiB

Taarifa ya Jumla:

Katika mistari hii, anayezungumziwa kama binadamu ni mji wa Babeli.

kwa sababu ya hofu ya maumivu yake

Nomino "hofu" na "mateso" zinaweza kuelezwa na misemo inayoweza kuonesha ni nani aliyehisi hofu na maumivu makali. "kwa sababu watahofia jinsi atakavyoteswa"

wakilia na kuomboleza kwa sauti

Hiki ndicho watakachokifanya wafanya biashara. "na watalia na kuomboleza kwa sauti"

mji ule mkuu uliovikwa kitani nzuri

Katika sura hii yote, Babeli inazungumziwa kama vile ni mwanamke. Wafanya biashara wanaizungumzia Babeli kama vile imevaa kitani nzuri kwa sababu watu wake walikuwa wamevaa kitani nzuri. "ule mji mkuu, ulio kama mwanamke aliyevaa kitani nzuri" au "ule mji mkuu, ambao wanawake wake walivaa kitani nzuri"

uliovikwa kitani nzuri

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "uliovaa kitani nzuri"

na kupambwa kwa dhahabu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na kujipamba mwenyewe kwa dhahabu" au "na kujipamba wenyewe kwa dhahabu" au "na kuvaa dhahabu"

vito vya thamani

"vito vinavyodhaminiwa"

lulu

Shanga nzuri na za dhamani. Zinaundwa ndani ya ganda la mnyama fulani mdogo aishiye baharini.

kipato chao kinatoka baharini

Msemo "kutoka baharini" inamaanisha kile wanachokifanya baharini. "wanaosafiri baharini kujikimu kimaisha" au "wanaosafiri baharini kwenda sehemu tofauti ili kufanya biashara ya vitu"