sw_tn/rev/18/04.md

1.2 KiB

Kauli Unganishi:

Sauti nyingine kutoka mbinguni inazungumza.

Taarifa ya Jumla:

Anayezungumziwa kama mtu ni mji wa Babeli, ambao unazungumziwa kama vile ni kahaba.

sauti nyingine

Neno "sauti" inamaanisha msemaji, ambaye huwezekana kuwa ni Yesu au Baba. "mtu mwingine"

Dhambi zake zimerundikana juu mpaka mbinguni

Sauti inazungumzia dhambi za Babeli kama vile ni vitu vinavyoweza kuunda rundo. "Dhambi zake ni nyingi sana ni kama rundo linalofika mbinguni"

ameyakumbuka

"akawazia" au "akaanza kuwa makini na." Hii haimaanishi kuwa Mungu alikumbuka jambo alilosahau.

Mlipeni kama alivyowalipa wengine

Sauti inazungumzia adhabu kana kwamba ni malipo. "Muadhibu kama alivyowaadhibu wengine"

mkamlipe mara mbili

Sauti inazungumzia adhabu kana kwamba ni malipo. "muadhibu mara mbili zaidi"

katika kikombe alichokichanganya, mchanganyishieni mara mbili kwa

Sauti inazungumzia kusababisha wengine kuteseka kama kuandaa divai yenye nguvu kwa ajili yao kunywa. "muandalie divai ya mateso ambayo ina nguvu mara mbili zaidi ya ile aliyowaandalia wengine" au "mfanyeni ateseke mara mbili zaidi ya alivyowatesa wengine"

mchanganyishieni mara mbili

Maana zinazowezekana ni 1)"andaa mara mbili ya kipimo" au 2)"ifanye kuwa na nguvu mara mbili zaidi"