sw_tn/rev/18/01.md

1.0 KiB

Kauli Unganishi:

Malaika mwingine ashuka toka mbinguni na kuzungumza. Huyu ni malaika tofauti na yule wa sura iliyopita, aliyezungumza kuhusu kahaba na mnyama.

Taarifa ya Jumla:

Anayezungumziwa hapa ni kama mtu ni mji wa Babeli.

Umeanguka, umeanguka, ule mji mkuu Babeli

Malaika anazungumzia Babeli kuangamizwa kama vile kuanguka.

ndege achukizaye

"ndege anayeudhi" au "ndege isyevutia"

mataifa yote

Mataifa ni njia nyingine ya kusema kwa watu wa mataifa hayo. "watu wa mataifa hayo"

yamekunywa mvinyo ya tamaa ya uovu wake

Hii ni ishara ya kushiriki katika tamaa zake za uasherati. "yamekuwa na uasherati kwama yeye" au "yamelewa na uasherati wake"

tamaa ya uovu wake

Babeli inazungumziwa kana kwamba ni kahaba aliyesababisha watu wengi wafanye dhambi pamoja naye. Hii inaweza kuwa na maana mara mbili: uasherati halisi na kuabudu miungu.

Wafanya biashara

Mfanya biashara ni mtu anayeuza vitu.

kwa nguvu ya maisha yake ya anasa

"kwa sababu alitumia pesa nyingi sana kwa ajili ya uasherati"