sw_tn/rev/12/07.md

863 B

Sasa

Yohana anatumia neno hili kubadili mwenendo wa maelezo yake kutambulisha kitu kingine kinachotokea katika maono yake.

joka

Hili lilikuwa tambaazi kubwa kali, kama mjusi. Kwa wayahudi ilikuwa ni alama ya uovu na machafuko. Joka pia linatambulika katika mstari wa 9 kama "ibilisi au Shetani"

Kwa hiyo haikuwepo tena nafasi mbinguni kwa ajili yake na malaika zake

"Kwa hiyo joka na malaika wake hawakuweza tena kukaa mbinguni"

Joka mkubwa ... akatupwa chini katika dunia ... na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye

"Mungu alilitupa joka na malaika wake toka mbinguni na kuwatuma duniani"

ule nyoka wa zamani aitwaye ibilisi au Shetani ambaye hudanganya dunia nzima

Hii taarifa inaweza kutolewa katika sentesi tofauti baada ya taarifa ya kutupwa duniani. "Hilo joka ni nyoka wa zamani anaye danganya ulimwengu. Anaitwa ibilisi au Shetani"