sw_tn/rev/09/05.md

877 B

Hawakupewa ruhusa

"Hawa" inamaanisha nzige.

hao watu

watu ambao walikuwa wanang'atwa na nzige.

bali kuwatesa tu

Hapa maneno "walipewa ruhusa" yanaeleweka. "lakini walipewa ruhusa kuwatesa"

kuwatesa

"kuwafanya wateseke maumivu makali"

kuwatesa kwa miezi mitano

Nzige wataruhusiwa kufanya hivi kwa miezi mitano.

kuumwa na nge

Nge ni mdudu mdogo wenye ncha kali yenye sumu mkiani. Kudungwa naye kunaweza kusababisha maumivu makali au hata kifo.

watu watatafuta kifo

Kifo kinazungumziwa kama mtu au kitu kinachoweza kufichwa. "watu watatafuta njia ya kufa" au " watu watajaribu kujiua"

hawatakipata

"hawataweza kupata njia ya kufa" au "hawataweza kufa"

Watatamani kufa

"watataka sana kufa" au "watatamani kwamba wafe"

kifo kitawakimbia

Yohana anazungumzia kifo kama vile ni mtu au mnyama anayeweza kukimbia. "hawataweza kufa" au "hawatakufa"