sw_tn/rev/01/07.md

869 B

Taarifa ya Jumla:

Katika mstari wa 7, Yohana ananakiri kutoka kitabu cha Danieli na Zekaria.

Kila jicho

Kwa kuwa watu huona kwa macho, neno "jicho" limetumika kuashiria watu. "kila mtu" au "watu wote"

pamoja na wote waliomchoma

"na wale waliomchoma pia watamuona"

waliomchoma

Mikono na miguu ya Yesu ilichomwa wakati aliposulibiwa msalabani. Hapa inamaanisha watu wakimuua. "walimuua"

mchoma

kutengeneza tundu katika

Alfa na Omega

Hizi ni herufi za kwanza na mwisho katika alfabeti ya Kigriki. Maana zinazowezekana ni 1) "yule aliyeanzisha vitu vyote na anayevileta mwisho vitu vyote" au 2)"yule ambaye alikuwepo na ataendelea kuwepo". "Yeye ni A na Z" au "mwanzo na mwisho"

ambaye anakuja

Atakayekuwapo baadaye ananenwa kama anayekuja.

asema Bwana Mungu

Baadhi ya lugha huweka "Bwana Mungu asema" mwanzoni au mwishoni mwa sentesi nzima.