sw_tn/psa/141/001.md

1.2 KiB

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

kulilia

"nakuomba msaada"

njoo upesi kwangu

Mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba Yahwe ni mtu aliyehitaji kuja kutoka sehemu nyingine kumsaidia. "Njoo upesi kunisaidia"

Nisikie ninapokuita

"Tafadhali nisikie ninapokuita" au "Nakuomba unisikie ninapokuita"

Na maombi yangu yawe kama uvumba

"Na maombi yangu yakupendeze kama harufu nzuri ya uvumba unavyowapendeza watu"

maombi yangu

Mwandishi wa zaburi anataka Yahwe kupendeza naye kwa sababu anaomba na kwa sababu ya maneno ya ombi lake.

mikono yangu iliyoinuka

"mikono niliyoinua juu." Mikon iliyo inuka ni njia nyingine ya kusema maombi. Watu waliinua mikono yao walipoomba au kumsifu Yahwe.

iwe kama sadaka ya jioni

iwe kama mnyama aliyechomwa katika madhabahu jioni. Mwandishi anazungumza kana kwamba anataka Yahwe apendezwe naye kama anavyopendezwa na wanaoleta wanyama kwa ajili ya sadaka. Anataka Yahwe apendezwe kwa sababu mwandishi wa zaburi anaomba au kwa sababu ya maneno ya ombi lake.