sw_tn/psa/114/001.md

853 B

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Israeli iliondoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa wageni

Mistari hii miwili ina usambamba, "Israeli" na "nyumba ya Yakobo" inamaanisha kitu kimoja na "Misri" na "watu wageni" inamaanisha watu wale wale.

nyumba ya Yakobo kutoka kwa wageni

Neno "nyumba" hapa linamaansiha familia au uzao. Kitenzi kinaweza kuwekwa kwa ajili ya huu msemo. "uzao wa Yakobo ukaondoka kutoka kwa watu wageni"

Yuda pakawa mahali pake patakatifu, Israeli ufalme wake

Maana zinazowezekana kwa ajili ya "Yuda" na "Israeli" ni 1) zinamaanisha nchi. "Nchi ya Yuda ikawa sehemu takatifu ya Yahwe, nchi ya Israeli ikawa ufalme wake" au 2) ni njia nyingine ya kusema watu wa Yuda na Israeli. "Watu wa Yuda wakawa miongoni mwa wale ambapo Yahwe aliishi, watu wa Israeli wakawa wale ambao aliwatala"