1.2 KiB
Dhambi za mababu yake zitajwe kwa Yahwe
Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Na ukumbuke dhambi za mababu zake, Yahwe"
na dhambi ya mama yake isisahaulike
Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Na usisahau dhambi ambazo mama yake alitenda"
Na hatia yao daima iwe mbele ya Yahwe
Hapa Daudi anazungumzia Yahwe kuwaza kuhusu hatia yao kana kwamba hatia yao ni kitu cha kimwili kilicho mbele yao. "Na Yahwe aendelee kufikiria kuhusu dhambi zao"
Yahwe akate kumbukumbu yao kutoka duniani
Daudi anatumia neno "dunia" kumaanisha watu wote wanaoishi duniani. Pia, msemo "kumbukumbu yao" inamaanisha watu kuwakumbuka baada ya kufa. "na Yahwe afanye kwamba watu duniani wasiwakumbuke"
mtu huyu hajawahi kuhangaika kuonesha uaminifu wowote wa agano
Hii inamaanisha yeye kuonesha uaminifu wa agano kwa watu. "mtu hakuhangaika kuonesha uaminifu wa agano kwa watu"
waliokandamizwa, wahitaji
Hii inamaanisha watu waliokandamizwa na wahitaji. "watu waliokandamizwa, watu wahitaji"
waliovunjika moyo
Hii inamaanisha watu waliovunjika moyo. "watu waliovunjika moyo" au "watu waliokata tamaa"
hadi kifo
"hadi wafe." Hii inamaanisha kuwa aliwatesa hadi walipokufa.