sw_tn/psa/102/009.md

693 B

Ninakula majivu kama mkate

Daudi angekuwa amekaa katika majivu kama kitendo cha kuomboleza, kwa hiyo majivu yangeanguka kwenye chakula chake. "Ninakula majivu kama ninavyokula mkate" au "Ninapoomboleza, majivu hudondoka kwenye mkate ninaokula"

na kuchanganya kinywaji changu na machozi

Daudi hakuchanganya kwa makusudi kinyaji chake na machozi; bali chozi lake lingedondoka katika kikombe chake wakati akiomboleza na kulia. "na machozi yangu yanadondoka kwenye kikombe ninachonywea"

umeniinua juu kunitupa chini

Mungu hajainua kiuhalisia mwili wa Daudi na kuutupa ardhini; bali Daudi anasema hivi kuelezea anachojisikia na kupitia. "ni kana kwamba umeniinua juu ili kunitupa chini"