sw_tn/psa/101/002.md

951 B

Nitatembea katika njia ya uaminifu

Hapa Daudi anazungumza kuhusu "kuishi" kana kwamba ni "kutembea." "Nitaishi kwa namna ambayo ni ya uaminifu na sawa" au "Nitaishi maisha yaliyo jaa uaminifu"

Nitatembea na uaminifu ndani ya nyumba yangu

Hapa Daudi anazungumza kuhusu "kuishi" kana kwamba ni "kutembea." Pia, Daudi anazungumzia kuhusu kuangalia nyumba yake kwa uaminifu , kana kwamba uaminifu ni kitu cha kimwili kinachokaa ndani ya nyumba yake. "Nitaichunga nyumba yangu kwa uaminifu"

Sitaweka uovu mbele ya macho yangu

"Uovu" ni nomino dhahania inayoweza kuandikwa kama msemo. Lahaja, "weka uovu mbele ya macho yangu," inamaanisha kuukubali. "Sitakubali mtu kufanya kisicho sawa mbele yangu"

haitang'ang'ania kwangu

Daudi anaelezea "uovu" kana kwamba ni kitu kinachoweza kumng'ang'ania. Hii inamaanisha ataepuka vitu viovu na watu wanaofanya vitu viovu. "Nitajiepusha kabisa na uovu"

ng'ang'ania

kushikilia kitu au mtu kwa nguvu.