sw_tn/psa/091/001.md

893 B

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Yeye anayeishi ... atabaki ... ya Mwenyezi

"Aliye juu, Mwenyezi, atawajali wote wanaoishi mahali anapoweza kuwalinda"

anayeishi katika kivuli cha Aliye juu

Neno "kivuli" ni sitiari ya ulinzi. "anayeishi mahali ambapo Aliye juu humlinda"

Aliye juu

Maneno "Aliye juu" yanamaanisha Yahwe.

atabaki katika kivuli cha Mwenyezi

Neno "kivuli" hapa ni sitiari ya ulinzi. "atabaki mahali ambapo Mwenyezi anaweza kumlinda"

Mwenyezi

yule mwenye uwezo na mamlaka juu ya kila kitu

Nitasema ya Yahwe

"Nitasema kumhusu Yahwe"

kimbilio lnagu na ngome yangu

"Kimbilio" ni sehemu ambapo mtu anaweza kwenda na kuwa na mtu au kitu kinachomlinda. "Ngome" ni kitu ambacho watu hutengeneza ili wajilinde wao na mali zao. Asafu anayatumia hapa kama sitiari ya ulinzi. "yule ambaye ninaweza kwenda kwake na atanilinda"