sw_tn/psa/090/011.md

800 B

Nani ajuaye ukali wa hasira yako, na gadhabu yako ambayo inalingana na kukucha wewe?

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kuwa hakuna mtu aliyepitia kikamilifu hasira ya Mungu. Kwa hiyo hakuna mtu anayemheshimu Mungu na kuogopa hasira yake watu wanapotenda dhambi. "Hakuna mtu anayejua ukali wa hasira yako. Kwa hiyo hakuna mtu anayeogopa gadhabu yako wanapotenda dhambi."

Geuka, Yahwe! Hadi lini?

Kumwomba Yahwe kutokuwa na hasira tena inazungumziwa kana kwamba mwandishi anataka Mungu ageuke kimwili kutoka katika hasira yake. "Yahwe, tafadhali usiwe na hasira na sisi tena'

Hadi lini?

Mwandishi anatumia swali kueleza kuwa anataka Mungu aache kuwa na hasira.

Kuwa na huruma kwa watumishi wako

Hapa "watumishi wako" inamaanisha watu wa Israeli. "Kuwa na huruma kwetu, watumishi wako"