sw_tn/psa/088/011.md

1.1 KiB

Je! Uaminifu wako wa agano utatangazwa kaburini, uaminifu wako katika sehemu ya wafu?

Maswali yote yanamaanisha kitu kimoja. Mwandishi anatumia maswali kusisitiza kuwa mtu aliyekufa hawezi kusifu uaminifu wa Mungu. "Hakuna atakaye tangaza uaminifu wako wa agano au uaminifu wako kutoka kaburini"

kaburini ... sehemu ya wafu ... gizani ... sehemu ya usahaulifu

Majina haya yote yanawakilisha mahali ambapo watu huenda baada ya kufa.

uaminifu wako katika sehemu ya wafu?

"Je! Uaminifu wako utatangazwa katika sehemu ya wafu?" au "Wale waliokufa hawatatangaza uaminifu wako."

Je! Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani, au haki yako katika sehemu ya haki?

Maswali yote yanamaanisha kitu kimoja. Mwandishi anatumia maswali kusisitza kuwa wale walio kufa hawawezi kupitiia au kutangaza mambo makuu ambayo Mungu hufanya. "Watu hawazungumzii kuhusu matendo yako ya ajabu na haki katika sehemu ya giza ya watu walio sahaulika."

au haki yako katika sehemu ya haki?

"Je! Haki yako itajulikana katika sehemu ya walio sahaulika?" au "Wale walio katika sehemu ya usahaulifi hawatajua kuhusu mambo ya haki unayofanya."