sw_tn/psa/088/009.md

764 B

Macho yangu yanachoka kutokana na taabu

Hapa "macho" yanawakilisha uwezo wa mtu kuona. Kwa macho yake kuchoka kutokana na taabu ni njia ya kusema kwamba matatizo yake yanamsababisha kulia sana hadi inakuwa kazi kwake kuona.

Ninanyosha mikono yangu kwako

"Ninainua mikono yangu kwako." Hiki ni kitendo kinachoonesha kuwa anamtegemea Mungu kabisa.

Je! Utafanya maajabu kwa wafu?

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kuwa kama Mungu akimwacha afe basi Mungu hataweza tena kufanya mambo ya ajabu kwa ajili yake. "Wewe hufanyi maajabu kwa awatu waliokufa."

Je! Wale waliokufa watafufuka na kukusifu

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kuwa kama Mungu akimwacha afe basi hataweza kumsifu Mungu tena. "Unajua kuwa waliokufa hawataweza kusimama na kukusifu"