sw_tn/psa/087/005.md

925 B

Kwa Sayuni itasemwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu watasema kuhusu Sayuni"

Kila mmoja wa hawa alizaliwa ndani yake

Watu kutoka mataifa mengine wanaomwabudu Yahwe wanazungumziwa kana kwamba walizaliwa Yerusalemu. "Ni kana kwamba watu hawa wote walizaliwa Yerusalemu"

ndani yake

Ilikuwa kawaida kuelezea miji kama mtu.

Aliye juu mwenyewe

Mwandishi anatumia kiwakilishi cha kujirudia "mwenyewe" kusisitiza kuwa Aliye juu ndiye anafanya hiki.

atamuimarisha

"ataifanya Yerusalemu kuwa imara"

Yahwe anaandika katika kitabu cha sensa cha mataifa

Yahwe kukubali kuwa watu kutoka mataifa mengine ni wake inazungumziwa kana kwamba yeye ni mfalme anayeandika majina ya watu wanaoishi katika mji wake.

Huyu hapa alizaliwa huko

"Huyu" inamaanisha watu kutoka mataifa ambayo mwandishi ametaja. Ingawa hawakuzaliwa kimwili Sayuni, wale wanaomfuata Mungu ni wakazi wa Mji wa Yerusalemu kiroho.