582 B
582 B
Fanya kwao ...kwa ajili ya dunia
Mwandishi anamwomba Mungu kuwashinda adui wa Israeli kama alivyofanya kipindi cha nyuma.
ulivyofanya kwa Midiani
Hapa "Midiani" inawakilishwa watu wa Midiani. "ulivyofanya kwa Wamidiani"
Sisera ... Yabini
Haya ni najina ya wanaume. Yabini alikuwa mfalme wa Hazori. Sisera alikuwa kamanda wa jeshi la Yabini.
mto Kishoni
Hili ni jina la mto kaskazini mwa israeli
Endori
Hili ni jina la mji kaskazini mwa Israeli,
wakawa kama mbolea kwa ajili ya dunia
Hii inamaanisha miili ya Sisera na Yabini haikuzikwa lakini iliachwa kuoza.