sw_tn/psa/075/004.md

1.3 KiB

Nilisema

Maana zinazowezekana ni 1) Mungu anazungumza au 2) Asafu anazungumza

Msiwe na kiburi ...Msiinue ... Msiinue ... msizungumze

Anaye zungumza anazungumza na watu wengi waovu.

na kwa waovu

"na nikasema kwa waovu"

Msiinue juu pembe

Asafu anazungumzia watu waovu kana kwamba ni wanyama wenye pembe vichwani mwao, wanonyosha shingo zao na kuweka vichwa vyao juu kutisha wanyama wengine. "Msiwe wajasiri" au "Msijivune jinsi mlivyo na nguvu"

Msiinue pembe yenu juu

Asafu anazungumzia watu waovu kana kwamba ni wanyama wenye pembe vichwani mwao, wanonyosha shingo zao na kuweka vichwa vyao juu kutisha wanyama wengine. "Kuweni waangalifu sana kutokuwa na majivuno kuwa mko bora zaidi ya Mungu"

na shingo yenye jeuri

Asafu anazungumzia watu waovu wanaomkaidi au kupingana na Mungu kana kwamba ni wanyama wenye pembe vichwani mwao, wanonyosha shingo zao na kuweka vichwa vyao juu kutisha wanyama wengine. "kwa kiburi"

Sio mashariki ... kuinuka kunakotokea

Asafu anamzungumzia yule anayeinua kana kwamba ndio tendo la kuinua. Anazungumzia pia Mungu kumpa nguvu na heshima mtu kana kwamba Mungu alikuwa akimnyanyua mtu kimwili. "Yule ambaye atakuinua hatakuwa mtu atokaye mashariki" au "Yule ambaye atakufanya kuwa na nguvu na kuwafanya watu wakuheshimu hatakuwa mtu anayetoka mashariki"