sw_tn/psa/068/004.md

1017 B

jina lake

Hii inamaanisha Mungu. "kwake"

yule anayeendesha katika sehemu za wazi

Uwepo wa Mungu katikati ya watu unazungumziwa kana kwamba anaendesha juu ya dunia katika farasi au kibandawazi.

Baba wa wasio na baba

Mungu anazungumziwa kama Mungu mwenye huruma anayekuwa kama baba kwa yatima. "Yule anayekuwa kama baba kwa watoto wasio na wazazi"

mwamuzi wa wajane

Mungu anazungumziwa kama Mungu anayewlinda wajane. "mlinzi wa wajane"

Mungu huwaweka wapweke katika familia

Mungu anazungumziwa kana kwamba huwaweka watu wapweke katika familia. "Mungu huwapa familia wale waiokuwa na mtu wa kuishi nao"

huwaleta nje wafungwa kwa kuimba

Mungu anazungumziwa kama yule anayewaongoza wafungwa kutoka katika vifungo vyao. "Mungu huwaweka huru wafungwa na huwafanya waimbe kwa furaha"

wakaidi

Hii inamaanisha watu wakaidi. "wale wanaokaidi dhidi yake"

nchi kavu

Adhabu ya Mungu kwa wakaidi inazungumziwa kana kwamba anawalazimisha kuishi katika jangwa lenye joto. "nchi kavu na yenye joto kali"