sw_tn/psa/068/001.md

1.0 KiB

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Acha Mungu ainuke

Mungu kuanza kutenda inazungumziwa kana kwamba anasimama. "Acha Mungu aanze kutenda"

acha adui zake watawanyike

"acha Mungu awafukuze adui zake"

Kama moshi unavyopeperushwa, ndivyo hivyo uwapeperushe

Adui wa Mungu wanazungumziwa kana kwamba ni moshi unaoweza kupeperushwa kwa urahisi na upepo. "Waondoe kama upepo unavyopuliza moshi"

kama nta inavyoyeyuka mbele ya moto

Adui wa Mungu wanazungumziwa kana kwamba ni nta inayoyeyuka kwa wepesi na moto. "wasababishe kupotea kama nta inavyoyeyuka mbele ya moto.

waovu

Hii inamaanisha watu waovu kwa ujumla.

wenye haki

Hii inamaanisha watu wenye haki kwa ujumla.

wafurahi na kushangilia

Hii inamaanisha kitu kimoja na inasisitiza kiasi cha furaha walichokuwanacho.