1.2 KiB
mataifa yalikasirika
Hapa neno "kukasirika" ni neno sawa mwandishi alilotumia katika 46:1 kuelezea maji ya bahari. Mwandishi anazungumzia uoga wa mataifa kana kwamba ni kusogea kwa fujo kwa bahari wakati wa dhoruba. "mataifa yanaogopa"
falme zilitikiswa
Hapa neno "kutikiswa" ni neno sawa ambalo mwandishi alitumia katika 46:1 kuelezea madhara ya tetemeko kwenye milima. Mwandishi anazungumzia kuangushwa kwa falme na majeshi kana kwamba tetemeko litawaangamiza. "majeshi yanapindua falme"
akainua sauti yake
"Mungu akainua sauti yake." Mwandishi anazungumzia "sauti" kana kitu amabcho mtu anaweza kuinua na kuweka hewani. Hii inamaanisha kwamba sauti inakua ya sauti zaidi. "Mungu alipaza sauti"
dunia ikayeyuka
Mwandishi anazungumzia dunia kama kitu, kama barafu, inayoweza kuyeyuka. Hapa "'dunia" inawakilisha binadamu, na kuyeyuka inawakilisha uoga. "watu wa duniani wanatetemeka kwa uoga"
Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu
Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni sehemu ambayo watu wanaweza kwenda kwa ajili ya ulinzi. "Mungu wa Yakobo anatupa ulinzi"
Mungu wa Yakobo
Maana zinazowezekana ni 1) "Mungu ambaye Yakobo alimwabudu" au 2) "Yakobo: ni njia nyingine ya kusema taifa la Israeli na inamaanisha "Mungu wa Israeli."