sw_tn/psa/044/001.md

989 B

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kihebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya wana wa Kora

"Hii ni zaburi ambayo wana wa Kora waliandika."

Maschili

Hii inaweza kuwa mtindo wa muziki.

Tumeskia kwa maskio yetu, Mungu

Neno "maskio" linaongeza mkazo kwa kauli waliosikia na kuelewa vitu ambavyo mwandishi anataka kueleza. Mwandishi anaeleza kauli hii kwa Mungu. "Mungu, tumesikia vizuri"

katika siku zao, katika siku za kale

Misemo yote hii miwili inatumia neno "siku" kumaanisha wakati ambao mababu wa watu wa Israeli walipokuwa hai.

Uliondoa mataifa

"Ulilazimisha watu wa mataifa mengine kuondoka"

kwa mkono wako

Hapa neno "mkono" linamaanisha nguvu ya Mungu. "kwa nguvu yako"

uliwapanda watu wetu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kusababisha Waisraeli kuishi katika nchi kana kwamba aliyokuwa akiwapanda katika udongo kama ambavyo angepanda mti. "uliwasababisha watu kuishi huko"