sw_tn/psa/040/005.md

764 B

Mawazo yako juu yetu hayahesabiki

"hakuna mtu awezaye kuhesabu vitu vyote unavyotuwazia"

hayahesabiki ... zaidi ya yanayoweza kuhesabika

Misemo hii inamaana sawa. Ya kwanza imeelezwa katika hali hasi na ya pili katika hali chanya.

Haupendezwi na dhabihu na sadaka

Hii ni kukuza kwa neno ili kuonesha kuwa vitu hivi havikuwa muhimu zaidi kwa Mungu. "Dhabihu na sadaka zingine sio vitu vinavyokufurahisha zaidi"

umefungua maskio yangu

Hapa "maskio" inamaanisha uwezo wa kusikia. "umeniwezesha kusikia amri zako"

hujaomba sadaka za kuchoma au sadaka za dhambi

Hii ni kukuza kwa neno ili kuonesha kuwa vitu hivi havikuwa muhimu zaidi kwa Mungu. "wanyama wanaotolewa kwenye madhabahu na sadaka zingine kwa ajili ya dhambi zetu sio unachotaka zaidi"