788 B
788 B
Sheria ya Mungu wake moyoni mwake
Hapa "moyo" unamaanisha hali yake ya ndani zaidi. "Anathamini amri za Mungu wake ndani mwake"
miguu yake haitateleza
Kushindwa kwake kumtii Yahwe kunazungumziwa kama kuteleza kwenye njia salama au kuanguka. "atatembea salama katika njia ambayo Mungu anataka atembee" au "atafanya kwa usalama vitu ambavyo Mungu anataka afanye"
Mtu mwovu ... mtu mwenye haki ... mtu mwovu
Hawa sio watu bayana. Inamaanisha aina hii ya watu kwa ujumla.
humtazama mtu mwenye haki
Hapa kutazama inaashiria kuwaangalia wenye haki ili kuwadhuru. "husibiri ili kumvamia mtu mwenye haki"
mkono wa mtu mwovu
Hapa "mkono" unawakilisha uwezo au nguvu. "uwezo wa mtu mwovu"
anapohukumiwa
Hii inamaanisha Yahwe kumhukumu mtu mwenye haki. "Yahwe atakapomhukumu"