sw_tn/psa/030/006.md

1002 B

Kwa ujasiri

Neno "ujasiri" ni nomino dhahania. Mwandishi anakumbuka kipindi alipokuwa akifanikiwa na kujihisi kuwa na ujasiri na salama. "Nilipokuwa na ujasiri" au "Nilipojihisi kuwa salama"

Sitatikiswa kamwe

Neno "kutikiswa" ni sitiari ya kushindwa. "Hakuna atakayenishinda"

kwa fadhila zako

Nomino dhahania "fadhila" inaweza kuelezwa kama kitenzi "pendelea" au kivumishi "huruma". "uliponipendelea" au "ulipokuwa na huruma kwangu"

umeniweka kama mlima imara

Usalama wa mwandishi unazungumziwa kana kwamba alikuwa mlima imara. "umenifanya salama kama mlima ulio juu"

ulipoficha uso wako

Hii ni lahaja. "ulipoacha kunisaidia" au "uliponikataa"

nilipata taabu

"niliogopa" au "nilikuwa na wasi wasi"

nikatafuta fadhila kutoka kwa Bawana wangu

Msemo "nikatafuta fadhila" inamaanisha kuomba msaada. "nilikuomba unisaidie"

kutoka kwa Bawana wangu

Mwandishi anamaanisha Yahwe katika hali ya mtu wa tatu. Inaweza kuelezwa katika hali ya mtu wa pili. "kutoka kwako, Bwana wangu"