sw_tn/psa/030/001.md

738 B

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo wakati wa kuweka wakfu hekalu

"Huu wimbo uliimbwa wakati hekalu linawekewa wakfu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

umeniinua

Mwandishi anazungumzia Mungu kumwokoa na kumwepusha na kufa kana kwamba Mungu amemuinua kutoka katika kisima kirefu. "umeniokoa"

umeinua nafsi yangu kutoka kuzimu

Kwa kuwa "kuzima" ilikuwa sehemu ambapo wafu huenda, inamaanisha kifo. "umeniepusha na kifo"

umeinua nafsi yangu

Hapa "nafsi yangu" inamaanisha mwandishi. "umenileta juu"

na kwenda chini kaburini

"Kaburi" linawakilisha kifo. "na kufa"