1.2 KiB
Usinikokote
Mungu kuwaadhibu inazungumziwa kana kwamba anawakokota kimwili. Katika sitiari hii, Yahwe anaweza kuwa anawakokota kwenda gerezani, uhamishoni, au kifoni. "Usinitoe"
ambao wanazungumza amani na majirani zao
Hapa "majirani" inamaanisha watu kwa ujumla. "wanazungumza kwa amani na watu wengine"
lakini wana uovu mioyoni mwao
Hapa "mioyo" inawakilisha akili au mawazo ya mtu. "lakini wanawaza kitu kiovu kuwahusu"
Wape kile ambacho matendo yao maovu yanastahili ... walipe kile ambacho uovu wao unadai
Misemo hii miwili ina maana sawa. Inatumika pamoja kusisitiza kuwa wanastahili kuadhibiwa na Mungu.
kazi ya mikono yao
Hapa "mikono" inawakilisha kile ambacho mtu amaefanya"
warudishie wanachostahili
"wape wanachostahili"
Kwa sababu hawaelewi ... usiwajenge tena
Haiko wazi kama mstari wa 5 unaeleweka kama kauli au ombi.
hawaelewi matendo ya Yahwe
Inadokezwa kuwa "hawaelewi" inamaanisha hawajali au kuheshimu kazi za Yahwe. "hawajali kwa heshima kile ambacho Yahwe amefanya"
kazi ya mikono yake
Hapa "mikono" inawakilisha kile ambacho Yahwe amefanya au kuumba. "alichoumba"
atawavunja chini na hatawajengea tena
Adhabu ya watu waovu inazungumziwa kana kwamba walikuwa wakijenga mji utakaoangamizwa.