sw_tn/psa/024/005.md

988 B

Atapokea baraka kutoka kwa Yahwe

Hapa hazungumziwi mtu yeyote bayana. Inamaanisha wale wenye mioyo safi waliotajwa kwenye mstari uliopita. Nomino dhahania ya "baraka" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "Yahwe atawabariki"

na haki kutoka kwa Mungu wa wokovu wake

Nomino dhahania ya "haki" inaweza kuelezwa kama "kwa haki." Na "wokovu" unaweza kuelezwa kama "okoa." "na Mungu atatenda kwa haki naye na kumwokoa"

Ndivyo kilivyo kizazi cha wale wanaomtafuta

Hapa "kizazi" inawakilisha watu kwa ujumla. "Watu wanaomtafuta wako hivi"

wale wanaomtafuta, wale wanautafuta uso wa Mungu wa Yakobo

Misemo yote miwili ina maana moja. Yote inamaanisha wale wanaoenda hekaluni kumwabudu Mungu. "wale wanaomkaribia Mungu, wao ndio wanaweza kumwabudu Mungu, yule ambaye sisi Waisraeli tunamwabudu"

wale wanaomtafuta

Kwenda hekaluni kumwabudu Yahwe inazungumziwa kana kwamba mtu anatafuta kwa uhalisia kumpata.

uso wa Mungu wa Yakobo

Hapa "uso" unamaanisha mtu mzima. "Mungu wa Yakobo"