sw_tn/psa/022/014.md

1.6 KiB

Ninamwagwa nje kama maji

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Ni kama mtu ananimwaga nje kama maji"

Ninamwagwa nje kama maji

Mwandishi anazungumzia kuhusu kujihisi kuchoka na munyonge kana kwamba alikuwa maji akimwagwa nje ya chupa

mifupa yangu yote imeteguka

"mifupa yangu yote iko nje ya sehemu zake." Inawezekana mwandishi yuko katika aina flani ya maumivu ya kimwili. Au anaweza kuwa anazungumzia maumivu ya hisia kana kwamba ni maumivu ya kimwili.

Moyo wangu ni kama nta ... sehemu zangu za ndani

Mwandishi anazungumzia kutokuwa na ujasiri kana kwamba moyo wake umeyeyuka kama nta. Hapa "moyo" unaashiria "ujasiri."

nta

kitu laini kinacho yeyuka kwa joto dogo.

ndani ya sehemu zangu za ndani

"ndani yangu"

Nguvu yangu imekauka kama kipande cha ufinyanzi

Mwandishi anazungumzia kujisikia mdhaifu kana kwamba nguvu yake ilikuwa kama kipande cha ufinyanzi kilichokauka na chepesi kuvunjika.

kipande cha ufinyanzi

kitu kilichoundwa kwa udongo wa kuoka kinachoweza kutumika ndani ya nyumba.

ulimi wangu unatokeza hadi kwenye paa ya mdomo wangu

"ulimi wangu unatokeza hadi juu ya mdomo wangu." Mwandishi anaweza kuwa anaelezea kiu yake kali. Au anaweza kuwa anaendelea kuzungumzia kuwa mdhaifu kana kwamba amekauka kabisa.

Umenilaza kwenye vumbi la mauti

Maana zinazowezekana kwa ajili ya "vumbi la mauti" ni 1) inamaanisha mtu kugeuka kuwa vumbi baada ya kufa. "Unataka kuniacha nife na niwe vumbi" au 2) ni njia ya kuzungumzia kaburi, ambayo inamaanisha Mungu anamsababisha mwandishi kufa. "Umenilaza kwenye kaburi langu"

Umenilaza

Aliyemlaza ni Mungu.