sw_tn/psa/022/009.md

797 B

Kwa kuwa

Mwandishi anatumia neno "Kwa" kuanza kueleza kwa nini amechanganyikiwa na kumwuliza Mungu kwa nini haji kumsaidia.

umenitoa kwenye tumbo

Hii ni njia ya kusema "umesababisha nizaliwe"

nilipokuwa katika kifua cha mama yangu

Hii inamaanisha kuwa amekuwa akimtumaini Yahwe tangu yuko mchanga. "hata tangu wakati nilipokunywa maziwa kutoka kifua cha mama yangu"

Nimetupwa kwako kutoka tumboni

Msemo "nimetupwa" ni njia ya kusema kuwa Yahwe amemtunza kana kwamba Yahwe alimpanga utoto kama mwana wake. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Ilikuwa kana kwamba umenipanga utoto tangu nilipozaliwa"

wewe ni Mungu wangu

Hii inadokeza kuwa Yahwe daima amekuwa akimctunza mwandishi. "wewe, Mungu, umenitunza"

tangu nimo tumboni mwa mama yangu

"tangu kabla sijazaliwa"