sw_tn/psa/022/006.md

930 B

mimi ni mnyoo na sio mtu

Mwandishi anajizungumzia kana kwamba alikuwa ni mnyoo. Hii inaonesha mkazo kuwa alijihisi hafai au kuwa watu walimtenda kana kwamba hana faida. "Lakini ni kama mimi ni mnyoo na sio binadamu"

aibu kwa wanadamu na kuchukiwa na watu

Misemo hii miwili inamaana sawa. Msemo "kuchukiwa na watu" unaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kila mtu anadhani sina faida na watu wananichukia"

wananidhihaki, wananifanyia mzaha; wanatikisa vichwa vyao kwangu

Misemo hii mitatu ina maana ya kukaribiana na inasisitiza jinsi watu walivyomdharau.

wanatikisa vichwa vyao kwangu

Hii inaelezea tendo ambalo watuwalitumia kumdhihaki mtu.

Anamtumaini Yahwe ... anamfurahia

Watu wanasema hivi kumdhihaki mwandishi. Hawaamani kweli kuwa Yahwe atamwokoa.

Acha amwokoe

"Acha Yahwe amwokoe"

kwa kuwa anamfurahia

Maana zinazowezekana ni 1) "kwa kuwa Yahwe anamfurahia" au 2) "kwa kuwa anamfurahia Yahwe"