930 B
930 B
mimi ni mnyoo na sio mtu
Mwandishi anajizungumzia kana kwamba alikuwa ni mnyoo. Hii inaonesha mkazo kuwa alijihisi hafai au kuwa watu walimtenda kana kwamba hana faida. "Lakini ni kama mimi ni mnyoo na sio binadamu"
aibu kwa wanadamu na kuchukiwa na watu
Misemo hii miwili inamaana sawa. Msemo "kuchukiwa na watu" unaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kila mtu anadhani sina faida na watu wananichukia"
wananidhihaki, wananifanyia mzaha; wanatikisa vichwa vyao kwangu
Misemo hii mitatu ina maana ya kukaribiana na inasisitiza jinsi watu walivyomdharau.
wanatikisa vichwa vyao kwangu
Hii inaelezea tendo ambalo watuwalitumia kumdhihaki mtu.
Anamtumaini Yahwe ... anamfurahia
Watu wanasema hivi kumdhihaki mwandishi. Hawaamani kweli kuwa Yahwe atamwokoa.
Acha amwokoe
"Acha Yahwe amwokoe"
kwa kuwa anamfurahia
Maana zinazowezekana ni 1) "kwa kuwa Yahwe anamfurahia" au 2) "kwa kuwa anamfurahia Yahwe"