sw_tn/psa/022/001.md

1.5 KiB

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Mapigo ya mbawala

Hii inaweza kumaanisha aina ya muziki.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Mungu wangu, Mungu wangu

Mwandishi anarudia "Mungu wangu" kusisitiza kuwa anatamani sana Mungu amsikie.

Mungu wangu, kwa nini umeniacha?

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kuwa anahisi kama vile Mungu amemwacha. Ni bora zaidi kuiacha hii kama swali. Inaweza pia kuwekwa kama kauli. "Mungu wangu, nahisi kama umeniacha!"

umeniacha

"umeniacha peke yangu"

Kwa nini uko mbali sana na kuniokoa na mbali na maneno yangu ya uchungu?

Mwandishi anatumia tena swali kusisitiza kuwa anahisi kama vile Mungu yuko mbali naye. Ni bora zaidi kuiacha hii kama swali. Inaweza pia kuwekwa kama kauli. "Uko mbali na kuniokoa na mbali na maneno ya uchungu wangu!"

mbali na maneno yangu ya uchungu

Mwandishi kuhisi kana kwamba Mungu hamsikilizi kunazungumziwa kana kwamba Mungu yuko mbali na maneno ya uchungu wake. Hapa "maneno" yanamaanisha chochote ambacho mwandishi anasema. "kwa nini hausikilizi ninapozungumza kwako kuhusu uchungu ninaoupitia" au "nimekuambia kuhusu mahangaiko yangu lakini haujaja kwangu"

mchana ... usiku

Mwandishi anatumia maneno "mchana" na "usiku" kumaanisha kuwa humwomba Mungu kila wakati.

siko kimya

Hii inaweza kuwekwa katika hali chanya. "Bado ninazungumza"