sw_tn/psa/018/007.md

906 B

Kisha ulimwengu ... ikatikiswa kwa sababu Mungu alikuwa na hasira

Mungu kuwa na hasira inazungumziwa kana kwamba ilikuwa ni tetemeko baya. "Mungu alikuwa na hasira sana hadi ikawa kama dunia ... ikatikisika"

ulimwengu ukatikisika na kutetemeka

Maneno "kutikisika" na "kutetemeka" yana maana sawa na yanasisitiza jinsi dunia ilivyotikisika. "nchi ikasogea huku na kule" au "ardhi ikasogea juu na chini" au "kulikuwa na tetemeko kali"

misingi ya milima pia ikatetemeka na kutikiswa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "misingi ya milima pia ikatetemeka na kutikisika"

Moshi ukatoka kwenye tundu zake za pua ... Makaa ikawashwa nao

Daudi anamzungumzia Yahwe kana kwamba alikuwa akipumua moto. Hii ni picha ya jinsi Mungu alivyokasirika.

moto ukatoka mdomoni mwake. Makaa ikawashwa nao.

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "moto ukatoka katika mdomo wake na kuwasha makaa"