sw_tn/phm/01/01.md

1.5 KiB

Paulo mfungwa wa Kristo Yesu, na Timotheo ndugu yetu kwa Filemoni

Lugha yako inaweza kuwa na njia maalum kwa mwandishi kujieleza kwa barua. "Sisi, Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na Timotheo, ndugu yetu, naandika hii barua kwa Filemoni."

mfungwa wa Kristo Yesu

"Mtu aliyefungwa kwa kufundisha kuhusu Yesu Kristo."

ndugu

Hapa hii inamaanisha mkristo mwenzake.

na mtendakazi mwenzetu

"Aliye, kama sisi, anakazi ya kueneza injili"

Afia dada yetu

Hii inamaanisha "Afia mkristo mwenzetu" au "Afia dada yetu kiroho"

Arkipo

Hili ni jina la mtu

Askari mwenzetu

Hapa ni "askari" ni fumbo inayomuelezea mtu anayepambana kwa kueneza injili. "Mwenzetu shujaa kiroho "au pia mpambanaji katika vita vya kiroho pamoja nasi."

neena iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo

"Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo awape neema na amani."Hii ni baraka. Neno "kwenu" ni kwa wengi na inarejea kwa watu wote waliosalimiwa na Paulo katika mstari wa 1 na 2.

Sentensi unganishi

Paulo amedhihirisha mara tatu kuwa yeye ni mwandishi wa barua hii. Timotheo alikuwa naye na aliandika maneno aliyoambiwa na Paulo. Paulo aliwasalimia waliokutana kusali katika nyumba ya Filemoni.

Maelezo ya jumla

Neno "mimi" linamaanisha Paulo. Filemoni ni mtu ambaye aliandikiwa barua hii. Sehemu zote zilizoandikwa "wewe" zinamuelezea Filemoni.

Maelezo ya jumla

Neno "yetu" inawajumuisha Paulo, Filemoni na waamini wa kanisa waliokuwa wakikutana kwenye nyumba ya Filemoni.

Baba yetu

Hiki ni cheo cha muhimu cha Mungu.