sw_tn/jas/04/01.md

1.5 KiB

Sentensi unganishi

Yakobo anawakemea waamini waliokosa unyenyekevu. Anawaonya kuwa makini na namna wanavyozungumza na watu wengine.

Maelezo ya jumla

Maneno "ninyi, wewe" imetumika kama wingi kuwaelezea waamini walioandikiwa na Yakobo.

ugovi unatoka wapi ... migogoro

Maneno "ugonvi, migogor" yanamaanisha kitu kimoja. Yakobo anayatumia kusisitiza kuwa nazungumzia juu ya mvutano kati ya watu.

ugonvi na migogoro

Ni tabia zinazotokea katika jamii

Haviinuki kutoka katika tamaa zenu mbaya zinazoleta vita

Yakobo anatumia swali kukemea hadhira yake. "ni kwa sababu mna tamaa mbaya" "kwa sababu mnatamani vitu vibaya"

Haviinuki kutoka katika tamaa zenu mbaya zinazoleta vita ndani ya washirika wenu?

Yakobo anazungumzia tamaa kama adui anayeleta vita kati ya waamini. kwa hali halisi ni watu ndio wenye tamaa hizi na kugombana wenyewe kwa wenyewe. "mnatamani maovu na mwishoni nmaumizana wenyewe kwa wenyewe"

Ndani ya washirika wenu

Yaweza kuwa na maana kuwa 1) kuna ugonvi kati ya waamini au 2) vita ambayo ni ugonvi upo ndani ya kila mwamini.

Mnauwa na mnafukuzia kile msichoweza kuwa nacho.

"mnauwa" inaelezea ni kwa kiasi gani watu wanaweza kufanya lolote baya ili wawezea kupata wanachokitaka. "Mnafanya uovu wa kila namna ili mpate msichoweza kukipata"

Mnapigana na kugombana

"kupigana na kugombana" zinamaanisha kitu kimoja. Yakobo anatumia kusisitiza namna ambavyo watu wanagombana wenyewe kwa wenyewe.

Mnaomba vibaya

Yaweza kuwa na maana kuwa 1) mnaomba mkiwa na nia mbaya au 2) mnaomba vitu ambavyo hampaswi kuomba au mnaomba vitu vibaya.