sw_tn/jas/02/05.md

1.3 KiB

Sikilizeni, ndugu zangu wapendwa

Yakobo anawachukulia wasomaji wake kama ndugu. "kuweni makini, ndugu zangu wapendwa"

Mungu hakuwachagua ... wampendao?

Yakobo anatumia swali kuwafundisha wasomaji wake wasiwe na upendeleo. "Mungu aliwachagua ... mpende yeye"

masikini

"watu masikini."

Kuwa tajiri katika imani

Kuwa na imani kubwa ni utajiri. "kuwa na imani thabiti kwa Kristo"

Warithi

Watu ambao Mungu aliwaahidi watairithi mali na utajiri kama vile watu warithipo toka kwa ndugu wa familia.

Lakini ninyi

Yakobo anaongea na hadhira yote.

mmewadharau masikini

"Mmewadhalilisha masikini"

Je, sio matajiri wanaowatesa ninyi

Hapa Yakobo anatumia maswali kuwasahihisha wasomaji wake. "Ni matajiri wanaowatesa ninyi."

tajiri

"watu matajiri"

wanaowatesa

"wanaowatendea mabaya"

Sio wao ... mahakamani?

Hapa Yakobo anatumia maswali kuwasahihisha wasomaji wake. " matajiri ndio wao ... mahakamani."

wanaowaburuza mahakamani

"wanaowapeleka kwa nguvu mahakamani na kuwashitaki kwa hakimu"

Hawalitukani ... mnaitiwa?

Hapa Yakobo anatumia swali kurekebisha na kufundisha wasomaji wake. "Matajiri ... mnaitiwa?

Jina zuri

"jina la Kristo" hii ni njia moja wapo ya kuelezea jina la Yesu. "Kristo ambalo kwalo mnaitiwa"

mnaitiwa

"mnajulikana kwalo"