sw_tn/isa/53/10.md

877 B

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kumfafanua mtumishi wa Yahwe.

ataona uzao wake

Hapa "uzao" una maana ya wale watu ambao Yahwe amewasamehe kwa sababu ya sadaka ya mtumishi.

atarefusha maisha yake

Hii inazungumzia kumfanya aishi kwa muda zaidi. "Yahwe atamfanya mtumishi wake kuishi tena"

kusudi la Yahwe litatimizwa kupitia kwake

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atatimiza kusudi lake kupitia mtumishi wake"

Baada ya mateso ya maisha yake

Hapa "maisha yake" ina maana ya mtumishi. "Baada ya mtumishi kuteseka"

ataona nuru

tafsiri nyingi zinaelewa "nuru" hapa kumaanisha uhai. Yaani, mtumishi atakuwa hai tena.

Mtumishi wangu mtakatifu

Hapa "wangu" ina maana ya Yahwe

atabeba udhalimu wao

"kubeba" hapa ina maana ya kubeba na inawakilisha mtumishi wa Yahwe kuchukua hatia ya dhambi yao. "atachukua hatia yao juu yake mwenyewe"