sw_tn/isa/52/09.md

823 B

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

enyi uharibifu wa Yerusalemu

Isaya anazungumzia uharibifu wa Yerusalemu kana kwamba ulikuwa mtu ambaye angeweza kushangilia. Hii inawakilisha watu wa Yerusalemu ambao walishindwa. "nyie watu ambao mnaishi miongoni mwa uharibifu wa Yerusalemu"

amemkomboa Yerusalemu

Hapa "Yerusalemu" inawakilisha watu. "amewakomboa watu wa Yerusalemu"

amafunua mkono wake mtakatifu

Hapa "mkono" inawakilisha nguvu ya Yahwe. Yahwe kuonyesha watu wote wa mataifa ya kwamba ni mtakatifu na mwenye nguvu inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa shujaa aliyetoa joho lake, kufunua mikono yake kwa ajili ya vita. "alionyesha utakatifu wake na nguvu yake kuu"

mataifa yote; dunia yote

Hapa "mataifa" na "dunia" inawakilisha watu wa mataifa yote katika dunia yote.