sw_tn/isa/49/21.md

866 B

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na Sayuni kana kwamba ilikuwa mwanamke.

Nani amezaa watoto hawa kwa ajili yangu?

Sayuni anazungumza na watu ambao wanrudi kuishi katika mji kana kwamba watu hao walikuwa watoto wake. Swali la Sayuni linaelezea mshangao wake ya kwamba watoto wengi sana sasa ni wa kwake.

Nilondolewa na kuwa tasa, nikahamishwa na kuachwa

Sayuni anajifafanua kama mwanamke asiyeweza kupata watoto zaidi. Anadokeza sababu ya mshangao wake mkubwa.

Nilondolewa na kuwa tasa

"Nilikuwa nikiomboleza juu ya watoto wangu waliokufa na kutoweza kupata wengine"

nikahamishwa na kuachwa

"Niliondoka, bila mume"

Nani amekuza watoto hawa? Tazama, niliachwa peke yangu; hawa wametoka wapi?

Tena, Sayuni anatumia maswali kuelezea mshangao wake. "Tazama, niliachwa peke yangu; sasa watoto hawa wote ambao sikuwakuza wamekuja kwangu"