sw_tn/isa/37/31.md

963 B

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa Yahwe kwa Hezekia.

waliobaki

"aliyesalia" ni sehemu ya kitu ambacho hubaki baada ya wengine kuondoka. Hapa ina maana ya watu ambao wamebaki Yuda.

nyumba ya Yuda

Hapa "nyumba" ya Yuda ina maana ya vizazi vyake. "vizazi vya Yuda"

atachipua tena mzizi na kuzaa matunda

Hii inazungumzia watu wa Yuda kuwa na mafanikio kana kwamba walikuwa mimea ambayo ingetoa mzizi na kuzaa matunda. "itafanikiwa kama mmea ambao huota mzizi na kuzaa matunda"

Kwa maana kutoka Yerusalemu aliyesalia atajitokeza; kutoka Mlima Sayuni waliokoka watakuja

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kusisitiza watu waliosalia ambao waliokoka.

Ari ya Yahwe wa majeshi itafanya hivi

Hii inazungumzia Yahwe kufanya kitu kwa sababu ya ari yake kana kwamba "ari" yake ilikuwa ikifanya tendo kihalisia. "Kwa sababu ya ari yake, Yahwe wa majeshi atafanya hivi" au "Yahwe wa majeshi atafanya hivi kwa sababu ya ari yake"