sw_tn/isa/29/22.md

1.5 KiB

nyumba ya Yakobo

Hapa "nyumba" inawakiliisha familia. "vizazi vya Yakobo"

ambao walimkomboa Abrahamu

Hii huenda ina maana ya pale Yahwe alipomwita Abrahamu kutoka katika nchi yake ya nyumbani na kumtuma katika nchi ya ahadi.

Yakobo hata ... uso wake ...atakapowaona watoto wake

Hapa "Yakobo" inawakilisha vizazi vyake. "Vizazi vya Yakobo havitakuwa tena ... nyuso zao ... wataona watoto wao"

wala uso wake kupauka

Hii ni lahaja ambayo ina maana ya hawatakuwa na hofu tena. "wala hawataogopa"

Lakini atakapowaona watoto wake, kazi ya mikono yangu

Hapa "mikono" inawakilisha nguvu na matendo ya Yahwe. "Watakapowaona watoto wote niliowapatia na yote niliyofanya"

watafanya jina langu kuwa takatifu

Hapa "jina" linawakilisha Yahwe. "wataniinua mimi"

Watafanya jina kuwa takatifu la Mtkatifu wa Yakobo

Hapa "jina" linawakilisha Yahwe. Yahwe anajitambua mwenyewe kama "Mtakatifu wa Yakobo". "Wataninua mimi, Mtakatifu wa Yakobo"

wa Mungu wa Israeli

Yahwe anajitambua mwenyewe kama "Mungu wa Israeli". "wa kwangu, Mungu wa Israeli"

Wale wanaopotoka katika roho

Hapa "roho" inawakilisha undani wa mtu. "Wale ambao wamekosea kwa kiile wanachowaza" au "Wale ambao wanakosea katika mtazamo wao"

watapata uelewa

Hii inaweza kufanywa waz zaidi kufafanua kile watakachoelewa. "wataanza kumuelewa Yahwe na sheria zake"

walalamishi watajifunza maarifa

Hii inaweza kuwekwa wazi kufafanua ni maarifa yapi watajifunza. "wale ambao wanalalamika wataanza kujua ya kwamba kile Yahwe anawafundisha ni cha kweli"