sw_tn/isa/29/20.md

1.1 KiB

Kwa maana wakatili watakoma

Kivumishi kiidogo "wakatili" kinaweza kuwekwa kama kivumishi. "Kwa maana watu wakatili watakoma" au "Kwa kuwa hapatakuwa tena na watu katili"

na mwenye dharau atatoweka

Kivumishi kidogo "mwenye dharau" kinaweza kuandikwa kama kitenzi. "na wale ambao hudharau watatoweka" au "na watu ambao hukejeli watapotea"

Wote wale ambao hupenda kutenda uovu wataondoshwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe ataondosha wote wale ambao hupenda kutenda uovu"

ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mhalifu

Hapa "neno" linawakilisha ushuhuda mahakamani. "ambao husem mahakamani ya kwamba mtu asiye na hatia ana hatia ya kufanya jambo baya"

Wanalaza mtego kwa ajili yake atafutaye haki katika lango na kuiweka haki chini kwa uongo mtupu

Watu waovu kufanya chochote wawezacho kumzuia mtu mwema inazungumzwa kana kwamba watu waovu waliweka mtego kama mwindaji akikamata mawindo. "Wanadanganya na kujaribu kuzuia wale ambao wanataka kufanya kiilicho haki na sahihi"

atafutaye haki katika lango

Malango ya mji mara kwa mara yalikuwa sehemu ambapo viongozi wa mji walifanya maamuzi rasmi.