sw_tn/isa/29/17.md

1.3 KiB

Lebanoni itageuzwa kuwa shamba, na shamba litakuwa msitu

Maana zaweza kuwa 1) huu ni uhalisi na Yahwe atasababisha maeneo ambapo miti iliota pori katika Lebanoni kuwa mashamba yanayozaa au 2) hii ni sitiari na misitu mikubwa ya Lebanoni inawakilisha wakandamizaji wenye nguvu, na mazao ambayo huota katika shamba na kuwa msitu ni watu wa kawaida ambao wanateseka. Hii ina maana Yahwe atawashusha wale ambao ni wenye nguvu, lakini atawainua wale ambao wanateseka.

Lebanoni itageuzwa kuwa shamba

Hapa "Lebanoni" inawakilisha msitu mkubwa wa mvinje wa Lebanoni. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mungu atageuza msitu mkubwa wa Lebanoni kuwa shamba"

kiziwi atasikia maneno ya kitabu, na macho ya kipofu yataona giza nene

Maana zaweza kuwa 1) huu ni uhalisi na Yahwe atasabisha watu viziwi kusikia na watu vipofu kuona au 2) hii ni sitiari ya kwamba Yahwe atawezesha watu kusikia na kuelewa ujumbe wake au 3) inaweza kumaanisha zote 1 na 2.

macho ya kipofu

Hapa "macho" yanawakilisha mti kamili. "wale ambao ni vipofu"

Waliokandamizwa watafurahi tena katika Yahwe, na maskini miongoni mwa watu watafurahi katika Mtakatiifu wa Israeli

Misemo hii miwili ina maana moja. "Maskini na watu waliokandamizwa watafurahi tena kwa sababu ya kile Yahwe , Mtakatifu wa Israeli, alichofanya"