sw_tn/isa/29/13.md

1.2 KiB

Watu hawa huja karibu na mimi kwa vinywa vyao na kuniinua mimi kwa midomo yao

Maneno "vinywa" na "midomo" inawakilisha kile watu wanasema. Hapa pia inawakilisha kusema kitu lakini sio kukimaanisha kihalisia. "Watu wa Yerusalemu wanavunga kuniabudu na kuniheshimu kwa kile wanachosema"

lakini moyo wao upo mbali na mimi

Hapa "moyo" ni neno linalowakilisha mawazo ya mtu na hisia. Watu kutokuwa na kujizatiti kwa Yahwe inazungumziwa kana kwamba mioyo yao ilikuwa mbali sana kutoka kwake. "lakini hawaniheshimu katika mawazo yao" au "lakini hawajizatiti kwangu kiukweli"

Heshima yao kwangu ni amri to ya watu ambayo imefundishwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Wananiheshimu tu kwa sababu hicho ndicho watu wanawaambia kufanya"

Kwa hiyo, tazama, nitaendelea kufanya jambo la ajabu katika hawa watu, ajabu baada ya ajabu

"Kwa hiyo, tazama na angalia! ninaenda kufanya mambo mazuri na ya ajabu miongoni mwako ambayo hutaweza kuyaelezea"

Hekima ya watu wenye hekima wao itatoweka, na uelewa wa watu wenye busara wao itapotea

Kauli hizi mbili zina maana moja. Yahwe kuonyesha ya kwamba watu wenye hekima hawawezi kuelewa au kufafanua kile Yahwe anafanya inazungumziwa kana kwamba hekima yao na uelewa utapotea.