sw_tn/isa/29/03.md

929 B

Nitapiga kambi dhidi yako

Neno "nitapiga" ina maana ya Yahwe. Hii inawakilisha Yahwe kusababisha jeshi la adui kuziingira Yerusalemu. "Nitaamuru jeshi la adui zako kukuzingira"

uzio ... kazi za kuzingira

"Uzio" ni mnara ambao majeshi hujenga kushambulia miji kwa kuta ndefu. Pia, "kazi za kuzingira" ina maana ya silaha za aina nyingine majeshi hujenga kushambulia miji.

Utawekwa chini

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Adui wako atakuleta chini" au "Adui wako atakushusha"

na utazungumza kutoka ardhini; usemi wako utakuwa chini kutoka mavumbini. Sauti yako itakuwa kama zimwi kutoka kwenye ardhi, na usemi wako utakuwa dhaifu sana kutoka mavumbini

Kauli hizi zote zina maana moja. Zinasisitiza ya kwamba watu ambao hapo awali walizungumza maneno ya kujivuna watakuwa dhaifu na kulia baada ya adui kuwashinda. "na utaweza tu kuonge kwa minong'ono dhaifu kama ya roho inayozungumza ambapo wafu huishi"