sw_tn/isa/29/01.md

966 B

Ole wa Arieli

Hapa "Arieli" inawakilisha watu ambao wanaishi katika mji wa Arieli. "Jinsi gani itakuwa vibaya kwa watu wa Arieli"

Arieli

Hili ni jina lingine kwa ajili ya Yerusalemu, na lina maana ya "madhabahu".

Daudi alipoweka kambi

"Daudi alikaa" au "Daudi aliishi"

Ongeza mwaka kwa mwaka; acha sikukuu ziwadie

"endelea kusherehekea sikukuu yako mwaka baada ya mwaka". Hili ni tamko la kejeli. Yahwe anawaambia watu kuendelea kusherehekea sikukuu zao ambapo wanatoa sadaka kwake, lakini anajua haitamzuia kuwaangamiza.

Lakini nitazingira

Neno "nitazingira" ina maana ya Yahwe. Hii inawakilisha Yahwe kusababisha jeshi la adui kuzingira Yerusalemu.

atakuwa

Hapa "atakuwa" ina maana ya Arieli, ambayo inawakilisha watu wa Arieli. "watu wa Arieli wata"

kulia na kuomboleza

Maneno "kulia" na "kuomboleza" ina maana moja na inasisitiza ukali wa maombolezo. "wataomboleza kwa uchungu"

kama Arieli

Jina la Arieli lina maana ya "madhabahu"