sw_tn/isa/27/12.md

1.3 KiB

Itakuja kuwa

Msemo huu unaweka alama kwa tukio muhimu ambalo litatokea.

katika siku hiyo

Hapa "siku" inawakilisha kipindi cha muda kwa ujumla.

Yahwe atapura

Yahwe kukusanya watu wake kuwarudisha kutoka mataifa ya kigeni katika nchi ya Israeli inazungumziwa kana kwamba alikuwa akipura mtama kugawanya nafaka kutoka kwa makapi.

kutoka Mto Frati, mpaka kwenye korongo kavu la mto la Misri

Isaya anataja Mto Frati na Korongo kavu la Misri kumaanisha ya kwamba Yahwe atawarudisha watu wa Israeli ambao walikuwa uhamishoni katika nchi karibu na maji hayo, yaani, Ashuru na Misri. Mto Frati ni kaskazini mashariki mwa Israeli, na Korongo Kavu la Misri ni kusini magharibi mwa Israeli.

korongo kavu la mto la Misri

"kijito kidogo cha Misri"

wewe ... utakusanywa mmoja baada ya mwingine

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atawakusanya mmoja mmoja"

tarumbeta kubwa itapulizwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "mtu atapulizwa tarumbeta kwa sauti"

wanaoangamia katika nchi ya Ashuru watakuja, na waliotengwa katika nchi ya Misri

Taarifa inayoeleweka inaweza kuwekwa wazi. "wale ambao wapo uhamishoni na kufa katika nchi ya Ashuru na nchi ya Misri watarudi katika nchi ya Israeli"

mlima mtakatifu

"mlima mtakatifu" ni Mlima Sayuni, katika Yerusalemu.